Trump sasa anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Korea kaskazini kisiwani Sentosa Singapore
Mkutano unaosubiriwa kwa hamu kati
ya rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea kaskazini Kim
Jong-un utafanyika katika hoteli moja kwenye kisiwa cha Sentosa,
Singapore, ikulu ya Marekani imethibitisha.
Mkutano huo wa kihistoria utafanyika Juni 12, lakini taarifa nyingi bado haizjathibitishwa.
Itakuwa mkutano wa kwanza kati ya kiongozi wa Korea kaskazini na rais aliyepo madarakani wa Marekani.
Siku ya Jumanne usiku Trump amesema 'mipango inaendelea vizuri'.
"Uhusiano mwingi unaundwa, majadiliano makubwa yanaendelea kabla ya safari," amewaambia waandishi.
Lakini
inavyoonekana ni kwamba watakaa katika hoteli tofauti Singapore, kwa
mujiu wa ripoti katika gazeti la Straits Times . Hoteli hizo mbili zipo
katika kisiwa kikuu .
Sentosa ni mojawapo ya visiwa 63 vya Singapore
Kim Jong-un: Kiongozi mpya mwenye umaarufu katika siasa za Dunia
Ghafla Kim Jong-un amekuwa kiongozi mpya mwenye umaarufu katika siasa za 2018.
Baada ya kuwa kando kwa miaka mingi, ameibuka kuwa kiongozi mwenye nguvu.
Viongozi kutoka China, Urusi, Syria Korea kusini na Marekani wote wamekutana au awanatarajiwa kukutana na Bwana Kim mwaka huu. Wanafuatana kwa msururu. Vladimir Putin amemualika aende Vladivostock Septemba na rais wa Syria Assad amesema pia angependa kuitembelea Pyongyang.
"Huu
ni mwanzo mpya wa kimataifa ulio tofuati kabisa kuliko tulivyoshuhudia
mnamo 2010, wakati Kim Jong Un alipojitokeza kama mtu asiyejulikana,
kijana aliyetazamiwa kuwa mrithi wa uongozi.
"Sasa akiwa
amejihami kwa silaha nzito, Kim anajitokeza kama kiongozi wa nchi
inayojitazama kama nchi yenye nguvu za nyuklia sambamba na nchi
nyingine duniani zenye silaha za nyuklia ikiwemo Marekani. " anasema
Jean Lee, aliyekuwa mhariri mkuu wa shirika la habari la Associated
Press Pyongyang.
Baada ya Kim Jong-un.kutangaza kuwa mapngo wake wa silaha umekamilika, alitangaza kuwa lengo lake kuu ni kushughulikia uchumi.
Na ili kuweza kufanya hivyo alihitaji kuunda uhusiano na kufufua urafiki wa zamani.
Kituo cha kwanza kilikuwa China, mshirika mkuu wa kibiashara wa Korea kaskazini.
Rasi
Xi Jinping alisaidia kuidhinisha shinikizo kamili la Donald Trump
mwishoni mwa 2017, na kukatiza bidhaa muhimu hatua ambayo iliipa
Pyongyang kichefu chefu. Haki miliki ya pichaAFPImage caption
Kim na rais Xi walipigwa picha wakati wa mkutano huo
Lakini sasa Kim safari haziishi. Ameizuru China mara mbili chini ya miezi miwili.
Ilikuwa na hisia zilizoibuka katika mkutano wa kihistoria mnamo Aprili katika mpaka wa Korea na kiongozi wa Korea kusini Moon Jae-in. Haki miliki ya pichaGetty ImagesImage caption
Bwana Moon na Kim walikumbatiana wakati ulimwengu ukitazama
Alichukua hatua nyingine kama hiyo na Moscow wiki
iliyopita. Aliyekuwa mkuu wa ujasusi wa Korea kaskazini Kim Yong-chol
alipokuwa njiani kwenda Marekani, Kim aliamua sasa kumkaribisha Waziri
wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov mjini Pyongyang. Korea Kusini yaiwekea vikwazo Korea Kaskazini
Ilikuwa ni ziara ya kwanza ya mwanadiplomasi amkuu wa Urusi katika muda unaozidi mwongo mmoja.
Huenda ni sadfa, lakini ni jambo ambalo halikumfurahisha Donald Trump.
Haki miliki ya pichaReutersImage caption
Ziara ya waziri wa Urusi Lavrov Pyongyang
So iwapo Washington ilidhani kwamba Korea kaskazini
imekwama , Kim Jong-un anatuma ujumbe na kudhihirisha hadharani nafasi
nyingine alizo nazo.
Amebadili sheria za mchezo. Mwaka jana alijigamba kwa uwezo wake wa nyuklia, sasa anazitumia kama silaha ya kidiplomasia.
Lakini suali kuu ni je Mchezo huu wa Korea kaskazini utakwishaje? Na ni kitu gani kitakachofanyika baada ya mkutano?
Watu 10 wafariki ajali ya treni na basi Kigoma, Tanzania
Watu 10 wamefariki katika ajali
iliyotokea baada ya basi la abiria lililogongana na treni eneo la Gungu
katika manispaa ya Kigoma Ujiji, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu, ajali hiyo ilitokea majira ya saa kumi na mbili na robo asubuhi.
Basi
hilo la abiria ambalo linamilikiwa na kampuni ya Prince hamida
linadaiwa kugongana na treni lilipokuwa linatoka Kigoma Mjini kwenda
Tabora.
Treni hiyo ya mizigo ilikuwa ikitoka Kazuramimba kwenda Kigoma Mjini.
Rais
wa Tanzania John Magufuli ametuma salamu za rambirambi na kuwtaaka
„wadau wote wa usalama barabarani kuchukua hatua madhubuti za kuzuia
ajali hizi."
"Vyombo husika, chukueni hatua kali kwa wote wanaokiuka sheria za usalama barabarani," amesema.
Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amesema eneo ilipotokea ajali hiyo hutokea ajali za aina hiyo mara kwa mara.
"Nimezungumza
na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania ( TRC ) na tumekubaliana
kuwa tuweke kizuizi ( barrier ) Katika eneo hili ambapo reli ikatiza
barabara," amesema.
„ Hii itasaidia sana kupunguza ajali za namna
hii. Mkurugenzi wa TRC Bwana Masanja Kadogosa amekubali ushauri huu
ambao Wananchi wengi wa Kigoma Mjini wamekuwa wakiutoa."
Hali ilivyo: Mazishi ya pacha Maria na Consolata Tanzania
Watu wengi wamejitokeza asubuhi ya
leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) eneo la Iringa katika
ibada maalumu ya kuwaaga pacha waliokuwa wameungana Maria na Consolata
waliofariki mwishoni mwa juma.
Miongoni mwa waliofika ni viongozi
mbali mbali wa dini na kiserikali.Baada ya ibada kutakuwa na maandamano
ya kuelekea katika makaburi ya Tosamaganga ambapo ndipo miili yao
itakapopumzishwa.
Askofu Jimbo Katoliki Njombe, Alfred Maluma
amesema vifo vya Pacha hao vinafaa kutumiwa na Watanzania kukumbushana
wajibu wao kwa watu wenye ulemavu.
Wameacha somo hilo, tuwajali watu wenye ulemavu hilo ndilo somo walilotuachia Maria na Cobsolata."
Amesema
Mungu aliwaumba pacha hao kwa mfano wa sura yake na akawapa uhai kwa
kipindi walichokuwa duniani. Vifo vya Maria na Consolata ambao walikuwa
ni wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Ruaha vimegusa wengi hasa kutokana na
ujasiri walioonyesha wakati wa uhai wao.
Vile vile watakumbukwa kwa ucheshi wao.
Pacha hao wameandaliwa jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili, misalaba miwili na watazikwa katika kaburi moja.
Mkuu wa Shirika la Maria Consolata, Jane Nugi
alikuwa ameambia gazeti la Mwananchi kwamba pacha hao waliamua eneo
ambalo watazikwa.
Alisema katika uhai wao walichagua kuzikwa kwenye eneo wanalozikwa viongozi wa kanisa Katoliki eneo hilo.
"Wakati wakiumwa walisema wangetamani kuhifadhiwa tunakohifadhiwa sisi hivyo watazikwa kwenye makaburi ya Tosamaganga," alisema. Pacha hao walifariki dunia wakiwa katika hospitali ya Iringa usiku wa kuamkia Jumamosi.
Kifo chao kiliwagusa wengi Tanzania, wengi wakituma salamu zao za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii.
Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli, ambaye mapema mwaka huu alikutana na pacha hao, alieleza kusikitishwa kwake na vifo vyao.
"Nimesikitishwa
na kifo cha Maria na Consolata. Nilipokwenda hospitali waliliombea
taifa. Walikuwa na ndoto ya kulitumikia taifa," aliandika Rais Magufuli
kwenye Twitter.
Maisha ya Maria na Consolata
Maria na Consolata Mwakikuti walizaliwa eneo la Ikonda, wilaya ya Makete kusini magharibi mwa Tanzania mwaka 1996.
Walisoma
shule ya msingi ya Ikonda kabla ya kujiunga na shule ya sekondari ya
Maria Consolata na baadaye wakasomea hadi kidato cha sita katika shule
ya Udzungwa wilaya ya Kilolo.
Septemba mwaka jana, baada ya kufaulu mtihani wa kidato cha sita, walijiunga na chuo kikuu cha kikatoliki cha Ruaha, Iringa.
Walianza
kuugua maradhi ya moyo na Desemba wakahamishiwa taasisi ya maradhi ya
moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es
Salaam ambako walilazwa kwa miezi miwili.
Wamekuwa wakitatizwa na afya tangu wakati huo. Walipofaulu mtihani wa kidato cha sita, walieleza furaha yao kuu baada ya kufaulu mtihani na kueleza ndoto zao.
"Tulipokea
matokeo yetu tukiwa kwenye mazingira ya nyumbani tu, tukiendelea na
shughuli zetu za kila siku, tukaambiwa matokeo yametoka na tumefanya
vizuri, tulikuwa tukiwaza kabla ya hapo, unajua kwenye mitihani ya
mwisho huwezi kujiamini sana," alieleza Consolata
Habari yako? karibu ktk blog yetu kwa kijifunza mambo mbalimbali, pia usisahau ku-comment kama unapenda tuendelee kukufunza.
LEO tutaangalia faida ya baadhi ya matunda katika miili yetu. sababu matunda ni muhimu katika mwili na pia utufanya tuwe na afya bora. zifuatazo ni faida ya baadhi ya matunda mwilini
FAIDA ZA TANGO
1. Kuzuia kisukari, kuboresha mfumo wa damu na kuondoa kolesteroli mwilini.
2. Chanzo kikubwa cha Vitamin B.
3. Kusaidia kutunza ngozi.
4. Kuongeza maji mwilini.
5. Kukata hangover.
6. Kuimarisha mmeng'enyo wa chakula mwilini.
7. Kuzuia saratani mwilini.
8. Kusaidia kupungua uzito.
9. Kuondoa maumivu na kuboresha viungo vya mwili.
10. Kuondoa harufu mbaya ya kinywa.
FAIDA ZA PAPAI
1. Kuua na kuondoa mazalia ya minyoo mwilini.
2. Kusaidia kutibu vidonda vya tumbo.
3. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula.
4. Majani yake huleta ahueni kwa wagonjwa wa saratani.
5. Kupunguza uvimbe (anti-inflammatory).
6. Kuboresha misuli na neva mwilini.
7. Kusaidia kumeng’enya protini.
8. Kuboresha kinga ya mwili.
9. Kuboresha macho.
10. Kuboresha mfumo wa hewa
FAIDA ZA UBUYU
1. Kuzuia uhalibifu na mikunjo ya ngozi.
2. Kusaidia katika kupunguza uzito wa mwili.
3. Kuimarisha moyo.
4. Kusafisha ini na kuondoa sumu.
5. Kiwango kikubwa cha vitamin C.
6. Chanzo cha madini ya Calcium.
7. Kuimarisha kinga ya mwili.
8. Kuimarisha figo.
9. Kuimarisha mifupa na meno.
10. Kuimarisha mfumo wa fahamu
FAIDA ZA EMBE
1. Kupunguza kiwango cha asidi mwilini.
2. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula.
3. Kurekebisha kiwango cha insulin.
4. Kuboresha macho.
5. Kusafisha damu.
6. Kuboresha ngozi.
7. Kuzuia saratani.
8. Kuimarisha kinga mwilini.
9. Kutibu joto kiharusi (heat stroke).
10. Kupunguza kiwango cha kolesteroli.
FAIDA ZA NANASI
1. Chanzo kikubwa cha vitamin A.
2. Kusaidia kumeng’enya chakula.
3. Inarekebisha mapigo ya moyo.
4. Kuimarisha mifupa ya mwili.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Inasaidia kuzuia mafua na homa.
7. Kuimarisha mfumo wa kinga.
8. Chanzo cha vitamin C.
9. Inapunguza uvimbe.
10. Kupunguza spidi ya kuzeeka kwa seli mwilini
FAIDA ZA NJEGERE
1. Kuzuia saratani ya tumbo.
2. Kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.
3. Chanzo kizuri cha protini.
4. Kuboresha ufanyaji kazi wa ini.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Kuboresha kinga ya mwili.
7. Inaleta nguvu mwilini.
8. Ina virutubisho vya nyuzi nyuzi.
9. Inazuia kuzeeka haraka.
10. Imejaa virutubishi vingi muhimu mwilini.
FAIDA ZA PILIPILI HOHO
1. Husaidia kupunguza uzito.
2. Kuboresha mzunguko wa damu.
3. Inapunguza kolesteroli mwilini
4. Kuzuia shinikizo la damu.
5. Ina kiwango kidogo cha kalori.
6. Nzuri kwa kuboresha macho.
7. Kuimarisha mfumo wa kinga.
8. Inatibu anemia.
9. Inazua saratani.
10. Kuboresha moyo.
Mgogoro wa visiwa vya China Kusini: China yasema matamshi ya Marekani ni ya 'kijinga'
China imetaja kuwa
matamshi ya 'kijinga' yanayotolewa na Marekani kwamba inawatishia na
kuwashurutisha majirani zake kupitia kupeleka silaha katika bahari ya
kusini mwa China
Jenerali wa ngazi ya juu nchini China alisema kuwa China ina haki ya kupeleka majeshi na silaha katika himaya yake.
Awali waziri wa Ulinzi nchini Marekani James Mattis alisema kuwa vitendo vya Beijing vilizua maswali mengi kuhusu malengo yake.
Mataifa sita yanapigania visiwa hivyo , lakini China imepiga
jeki madai yake kwa kujenga katika visiwa hivyo mbali na kupiga doria.
Jenerali Mattis alitoa matamshi hayo katika mkutano wa usalama nchini Singapore.
Akizungumza
katika mkutano huohuo Luteni jenerali wa China He Lei alisema:
Matamshi yoyote ya 'kijinga' kutoka mataifa mengine hayawezi kukubalika.
Jenerali
He alisema hatua ya Bejing kupeleka wanajeshi wake ni kutokana na sera
yake ya kujilinda , akiongezea kuwa lengo lao kuu ni kuzuia uvamizi
wowote
''Ukiwa katika himaya yako unaweza kupeleka majeshi na silaha''.
Aliongezea: Tunachukulia taifa lolote linalojaribu
kupiga makelele kuhusu hatua hii kama taifa linalojaribu kuingilia
maswala yetu ya ndani.
Jenerali Mattis alisema kuwa China
ilipekeka zana za kijeshi na makombora ya kudungua ndege katika maeneo
ya visiwa hivyo vilivyopo kusini mwa bahari ya China.
Alisema kuwa lengo la China kupeleka vifaa hivyo na wanajeshi ni kuwatishia na kuwashurutisha majirani zake
Haki miliki ya pichaReutersImage caption
Bejing imekuwa ikivibadilisha visiwa hivyo kuwa kambi zake za kijeshi
Habari yako? leo nitaeleza jinsi ya kupiga window 7 kutoka kwenye cd. nifatiliee kwa makini ili uweze kupata ujuzi huu.
HATUA KWA HATUA Ingiza CD yako katika
DVD-ROOM ya mashine yako kisha subiri CD yako isome ikisha soma Restart
mashine yako kisha bonyeza Boot Button, hapa kila mashine huwa
zinatofautiana ila nyingi ni F8, F10 au F12, so angalia mashine yako
boot button yake ni ipi.
Kama itagoma usichoke rudia tena ila ikikubali utaona kama pichani hapo juu
Fanya machaguo sahihi
hapo katika Lugha, Time na type ya keyboard hiyo kwenye picha mimi ndo
huwa naitumia wakati wote sijawahi kubadilisha, kisha bonyeza Next
Utaona muonekano kama huo juu pichani sasa bonyeza Install Now
Weka tiki katika kibox ili kukubaliana na sheria za microsoft kisha bonyeza next ili kuendelea
Bonyeza Upgrade kama ulikuwa na Windows 7 na unataka kuibadilisha...Au bonyeza Custom (advanced) huna Windows 7 na unaweka windows 7 upya
Chagua Drive kama ni (C:) AU (D:) ambayo unataka kuweka windows 7.Bonyeza Drive options (advanced) kama
unataka kutengeneza Partiton (Kuigawanya hard disk ) Kisha bonyeza
Next, sasa windows yako itaanza mchakato wake wa kujiweka katika mashine
yako tazama picha hapa chini.
Baada ya michakato hiyo mashine yako itajizima na kujiwasha usiogope bado ipo katika mchakato tazama picha hapa chini
Ikishajiwasha
itaendelea na mchakato wa setup iliyobakia itachukua muda kidogo wenda
ikazidi ule muda wa mwanzo lakini usijali itamaliza kisha itajizima na
kujiwasha kwa mara ya pili.
ikishawaka
sasa itakupa chaguo la kuandika jina unaweza kuandika jina lolote
ulipendalo pia ukipenda unaweza kuweka na Password lakini kama
hautopenda andika jina tu kisha bonyeza next, wenda ikakuomba Keys chukua hapa kama hauna lakini pia unaweza kubonyeza next bila kuweka ila itakuja kukuomba baadae
Bonyeza next kisha set vitu hivi chini pichani kama utakavyopenda wewe
Mpaka kufikia hapo tayari Computer yako kwa kutumika. Asante
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.