Recent News

Joh Maker – Chekecha

Joh Maker – Chekecha

                           
https://yingamedia.com/wp-content/uploads/2018/06/joh-maker-chekecha.jpg

Share:

Ellymaizer X Super Newe – Mbuke

Download Audio: Ellymaizer X Super Newe – Mbuke


 
https://fanburst.com/yingaboy/ellymaizer-x-super-newe-mbuke/download


Share:

Trump sasa anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Korea kaskazini kisiwani Sentosa Singapore

Trump sasa anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Korea kaskazini kisiwani Sentosa Singapore

 

Mkutano unaosubiriwa kwa hamu kati ya rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un utafanyika katika hoteli moja kwenye kisiwa cha Sentosa, Singapore, ikulu ya Marekani imethibitisha.
Mkutano huo wa kihistoria utafanyika Juni 12, lakini taarifa nyingi bado haizjathibitishwa.
Itakuwa mkutano wa kwanza kati ya kiongozi wa Korea kaskazini na rais aliyepo madarakani wa Marekani.
Siku ya Jumanne usiku Trump amesema 'mipango inaendelea vizuri'.
"Uhusiano mwingi unaundwa, majadiliano makubwa yanaendelea kabla ya safari," amewaambia waandishi.
Lakini inavyoonekana ni kwamba watakaa katika hoteli tofauti Singapore, kwa mujiu wa ripoti katika gazeti la Straits Times . Hoteli hizo mbili zipo katika kisiwa kikuu .
Sentosa ni mojawapo ya visiwa 63 vya Singapore

Kim Jong-un: Kiongozi mpya mwenye umaarufu katika siasa za Dunia
Ghafla Kim Jong-un amekuwa kiongozi mpya mwenye umaarufu katika siasa za 2018.
Baada ya kuwa kando kwa miaka mingi, ameibuka kuwa kiongozi mwenye nguvu.
Viongozi kutoka China, Urusi, Syria Korea kusini na Marekani wote wamekutana au awanatarajiwa kukutana na Bwana Kim mwaka huu.

Wanafuatana kwa msururu. Vladimir Putin amemualika aende Vladivostock Septemba na rais wa Syria Assad amesema pia angependa kuitembelea Pyongyang.
"Huu ni mwanzo mpya wa kimataifa ulio tofuati kabisa kuliko tulivyoshuhudia mnamo 2010, wakati Kim Jong Un alipojitokeza kama mtu asiyejulikana, kijana aliyetazamiwa kuwa mrithi wa uongozi.
"Sasa akiwa amejihami kwa silaha nzito, Kim anajitokeza kama kiongozi wa nchi inayojitazama kama nchi yenye nguvu za nyuklia sambamba na nchi nyingine duniani zenye silaha za nyuklia ikiwemo Marekani. " anasema Jean Lee, aliyekuwa mhariri mkuu wa shirika la habari la Associated Press Pyongyang.
Baada ya Kim Jong-un.kutangaza kuwa mapngo wake wa silaha umekamilika, alitangaza kuwa lengo lake kuu ni kushughulikia uchumi.
Na ili kuweza kufanya hivyo alihitaji kuunda uhusiano na kufufua urafiki wa zamani.
Kituo cha kwanza kilikuwa China, mshirika mkuu wa kibiashara wa Korea kaskazini.
Rasi Xi Jinping alisaidia kuidhinisha shinikizo kamili la Donald Trump mwishoni mwa 2017, na kukatiza bidhaa muhimu hatua ambayo iliipa Pyongyang kichefu chefu.
Haki miliki ya picha AFP
Image caption Kim na rais Xi walipigwa picha wakati wa mkutano huo
Lakini sasa Kim safari haziishi. Ameizuru China mara mbili chini ya miezi miwili.
Ilikuwa na hisia zilizoibuka katika mkutano wa kihistoria mnamo Aprili katika mpaka wa Korea na kiongozi wa Korea kusini Moon Jae-in.
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Bwana Moon na Kim walikumbatiana wakati ulimwengu ukitazama
Alichukua hatua nyingine kama hiyo na Moscow wiki iliyopita. Aliyekuwa mkuu wa ujasusi wa Korea kaskazini Kim Yong-chol alipokuwa njiani kwenda Marekani, Kim aliamua sasa kumkaribisha Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov mjini Pyongyang.
Korea Kusini yaiwekea vikwazo Korea Kaskazini
Ilikuwa ni ziara ya kwanza ya mwanadiplomasi amkuu wa Urusi katika muda unaozidi mwongo mmoja.
Huenda ni sadfa, lakini ni jambo ambalo halikumfurahisha Donald Trump.
Haki miliki ya picha Reuters
Image caption Ziara ya waziri wa Urusi Lavrov Pyongyang
So iwapo Washington ilidhani kwamba Korea kaskazini imekwama , Kim Jong-un anatuma ujumbe na kudhihirisha hadharani nafasi nyingine alizo nazo.
Amebadili sheria za mchezo. Mwaka jana alijigamba kwa uwezo wake wa nyuklia, sasa anazitumia kama silaha ya kidiplomasia.
Lakini suali kuu ni je Mchezo huu wa Korea kaskazini utakwishaje? Na ni kitu gani kitakachofanyika baada ya mkutano?
  :SOURCE;- BBC SWAHILI
Share:

Watu 10 wafariki ajali ya treni na basi Kigoma, Tanzania

Watu 10 wafariki ajali ya treni na basi Kigoma, Tanzania


Watu 10 wamefariki katika ajali iliyotokea baada ya basi la abiria lililogongana na treni eneo la Gungu katika manispaa ya Kigoma Ujiji, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu, ajali hiyo ilitokea majira ya saa kumi na mbili na robo asubuhi.
Basi hilo la abiria ambalo linamilikiwa na kampuni ya Prince hamida linadaiwa kugongana na treni lilipokuwa linatoka Kigoma Mjini kwenda Tabora.
Treni hiyo ya mizigo ilikuwa ikitoka Kazuramimba kwenda Kigoma Mjini.
Rais wa Tanzania John Magufuli ametuma salamu za rambirambi na kuwtaaka „wadau wote wa usalama barabarani kuchukua hatua madhubuti za kuzuia ajali hizi."
"Vyombo husika, chukueni hatua kali kwa wote wanaokiuka sheria za usalama barabarani," amesema.
Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amesema eneo ilipotokea ajali hiyo hutokea ajali za aina hiyo mara kwa mara.
"Nimezungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania ( TRC ) na tumekubaliana kuwa tuweke kizuizi ( barrier ) Katika eneo hili ambapo reli ikatiza barabara," amesema.
„ Hii itasaidia sana kupunguza ajali za namna hii. Mkurugenzi wa TRC Bwana Masanja Kadogosa amekubali ushauri huu ambao Wananchi wengi wa Kigoma Mjini wamekuwa wakiutoa."

Share:

Hali ilivyo: Mazishi ya pacha Maria na Consolata Tanzania


Hali ilivyo: Mazishi ya pacha Maria na Consolata Tanzania

 

 

Watu wengi wamejitokeza asubuhi ya leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) eneo la Iringa katika ibada maalumu ya kuwaaga pacha waliokuwa wameungana Maria na Consolata waliofariki mwishoni mwa juma.
Miongoni mwa waliofika ni viongozi mbali mbali wa dini na kiserikali.Baada ya ibada kutakuwa na maandamano ya kuelekea katika makaburi ya Tosamaganga ambapo ndipo miili yao itakapopumzishwa.
Askofu Jimbo Katoliki Njombe, Alfred Maluma amesema vifo vya Pacha hao vinafaa kutumiwa na Watanzania kukumbushana wajibu wao kwa watu wenye ulemavu.
Wameacha somo hilo, tuwajali watu wenye ulemavu hilo ndilo somo walilotuachia Maria na Cobsolata."
Amesema Mungu aliwaumba pacha hao kwa mfano wa sura yake na akawapa uhai kwa kipindi walichokuwa duniani. Vifo vya Maria na Consolata ambao walikuwa ni wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Ruaha vimegusa wengi hasa kutokana na ujasiri walioonyesha wakati wa uhai wao.
Vile vile watakumbukwa kwa ucheshi wao.
Pacha hao wameandaliwa jeneza moja lenye mfumo wa watu wawili, misalaba miwili na watazikwa katika kaburi moja.

Mkuu wa Shirika la Maria Consolata, Jane Nugi alikuwa ameambia gazeti la Mwananchi kwamba pacha hao waliamua eneo ambalo watazikwa.
Alisema katika uhai wao walichagua kuzikwa kwenye eneo wanalozikwa viongozi wa kanisa Katoliki eneo hilo.
"Wakati wakiumwa walisema wangetamani kuhifadhiwa tunakohifadhiwa sisi hivyo watazikwa kwenye makaburi ya Tosamaganga," alisema.
Pacha hao walifariki dunia wakiwa katika hospitali ya Iringa usiku wa kuamkia Jumamosi.
Kifo chao kiliwagusa wengi Tanzania, wengi wakituma salamu zao za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii.
Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli, ambaye mapema mwaka huu alikutana na pacha hao, alieleza kusikitishwa kwake na vifo vyao.
"Nimesikitishwa na kifo cha Maria na Consolata. Nilipokwenda hospitali waliliombea taifa. Walikuwa na ndoto ya kulitumikia taifa," aliandika Rais Magufuli kwenye Twitter.

Maisha ya Maria na Consolata

Maria na Consolata Mwakikuti walizaliwa eneo la Ikonda, wilaya ya Makete kusini magharibi mwa Tanzania mwaka 1996.
Walisoma shule ya msingi ya Ikonda kabla ya kujiunga na shule ya sekondari ya Maria Consolata na baadaye wakasomea hadi kidato cha sita katika shule ya Udzungwa wilaya ya Kilolo.
Septemba mwaka jana, baada ya kufaulu mtihani wa kidato cha sita, walijiunga na chuo kikuu cha kikatoliki cha Ruaha, Iringa.
Walianza kuugua maradhi ya moyo na Desemba wakahamishiwa taasisi ya maradhi ya moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam ambako walilazwa kwa miezi miwili.
Wamekuwa wakitatizwa na afya tangu wakati huo.
Walipofaulu mtihani wa kidato cha sita, walieleza furaha yao kuu baada ya kufaulu mtihani na kueleza ndoto zao.
"Tulipokea matokeo yetu tukiwa kwenye mazingira ya nyumbani tu, tukiendelea na shughuli zetu za kila siku, tukaambiwa matokeo yametoka na tumefanya vizuri, tulikuwa tukiwaza kabla ya hapo, unajua kwenye mitihani ya mwisho huwezi kujiamini sana," alieleza Consolata
Share:

Harmonize Ft. Diamond Platnumz – Kwa Ngwaru

DOWNLOAD : Harmonize Ft. Diamond Platnumz – Kwa Ngwaru

 

Download

Share:

DIAMOND PLATNUMZ, HARMONIZE, RICH MAVOKO, RAYVANNY - ZILIPENDWA

DOWNLOAD WIMBO WA ZILIPENDWA BY WCB


Download
Share:

slide

MPYA

Popular Posts

Powered by Blogger.

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Author Details

Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.

Breaking

Fashion

News

Food

Sports

Food

Technology

Featured

Videos

Labels

Sponsor

AD BANNER

About Me

authorHello, my name is Jack Sparrow. I'm a 50 year old self-employed Pirate from the Caribbean.
Learn More →

Connect With us

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Blogger templates